Pages

Search This Blog

michuzi, MK,HAKI NGOWI, BONGO CELEBRITY, WATANZANIA, NGURUMO

Tuesday, 3 August 2010

Fernando Torrez Nitabaki Liverpool Daima







The Spain international, who returned to training yesterday after winning the World Cup in South Africa, has been the subject of persistent speculation.

However, the 26-year-old has moved to quash suggestions he was ready to move on.

"I am really happy to be back, really happy to stay with all my team-mates," he said.

"My commitment and loyalty to the club and to the fans is the same as it was on my first day when I signed.

"I am looking forward to the challenge ahe

Liverpool striker Fernando Torres has pledged his future to the club after insisting his "commitment and loyalty is the same as it was on my first day when I signed".


"I am really happy to be back, really happy to stay with all my team-mates," he said.




Na Abdallah Shelufumo

Thursday, 5 November 2009

50 Cent ready to take Kanye West's hip hop title after his recent VMAs drama


bifu bibu tuuuuuuu.......... eenh, pata hiii sasa

tujiunge na zefumo





Rapper 50 Cent has said he's ready to take Kanye West's hip hop title after his recent VMAs drama.


The 34-year-old vowed two years ago to give up rap if Kanye beat him to number one but the star has now said it's "cool to hate Kanye" at the moment.


Kanye, 32, was criticised for interrupting Taylor Swift's acceptance speech at the recent VMAs to say that Beyonce should have won the award.


50 Cent said: "Taylor is 17. She could be my child. Kanye may not have grown up in the space where you could have a child that early, but where I'm from, it could have happened.


"I could have a child her age right now. So it makes me feel different about the whole scenario. I don't think he had that in mind. I think he was just saying that he felt as an actual artist, and it's a mistake.


"He's paying for it now. I don't know how much damage it does, but it looks pretty bad from here. What do you do after that to make people sympathetic to you?"


He added: "Kanye was the underdog coming around under 50 Cent, and now he's becoming this guy who has so much arrogance that it's cool to hate Kanye West right now."

ndo vile yani bifu kwenda mbele.

chanzo na Abdallah Shelufumo




Rapper 50 Cent has 'lost a few million' in the economic crisis

mwanamuziki tajiri ndani ya sayari ya mziki.








Rapper 50 Cent has admitted he has "lost a few million" in the recent economic crisis.


The 34-year-old star has an estimated fortune of £500 million and is starring in new movie Dead Man Running.


He said: "Hey, if you don't lose some money in this recession it means you didn't have enough to start off with. Sure I lost a few [million] but that's just because I have so much. This is a time that will sort the strong from the weak."


However, that doesn't mean the rapper is cutting back on important things such as security.


He said: "I spend £20,000 a week on security. My home is surrounded by cameras. I need surveillance not only to look out for me but also to protect me. You get all these crazy lawsuits and I need cameras to check on things."


source with Abdallah Shelufumo

Sunday, 18 October 2009

wishing you Happy birthday and more to come abdallah

From Zefumo to Abdallah Shelufumo

On your birthday I wish you much pleasure and joy;
I hope all of your wishes come true.
May each hour and minute be filled with delight,
And your birthday be perfect for you!

Here's another year of experience






Pongezi kwa ngugu yetu Abdallah Shelufumo kwa kuzaliwa tena leo hii.

Blog yetu ya Zefumo ilikua pamoja bega kwa bega pamoja na mdau huyu ambaye vilevile ndio Mkurugenzi wa Blog hii ktk kufurahi siku ya kuzaliwa kwake.

Baadhi ys picha zilinazomuonesha Mdau mwenyewe hapo chini



Masanja anadai wahenga wanasema 'nchungaji mashuhuli kikwapa luwadudi" yaani

kazaliwa Abdallah Shelufumo kazaliwa Zefumoblogspot.

Picha zote na Zefumo.blogspot.com





Tuesday, 13 October 2009

In those dayz


kipindi hicho shuja wetu wa tanzania na Afrika.



[JK.Nyerere.jpg]







Ila mazee tumetoka mbali, au unaniambiaje kilo.

zefumo iko pamoja na watanzania katika kuhitimisha maadhimishi ya kumbukumbu ya shujaa wa Afrika.
na Shelufumo



The memorial of Mwalimu Nyerere


Maisha ya Julius Nyerere

Sehemu ya Kwanza: Kuzaliwa na Malezi
Julius Kambarage Nyerere alizaliwa mwezi wa nne, tarehe kumi na mbili, mwaka elfu moja, mia tisa na ishirini na mbili katika nchi ya Tanganyika, na alikufa mwezi wa kumi, tarehe kumi na nne, mwaka elfu moja, mia tisa, tisini na tisa katika mji wa London. Alizaliwa mjini Butiama, karibu na pwani ya mashariki ya Ziwa la Victoria. Nyerere alikuwa mmoja wa watoto ishirini na sita wa babake, Nyerere Burito. Babake alikuwa kiongozi wa kabila la Zanaki na alikuwa na wake wawili. Pia babake alikuwa na fedha nyingi lakini hakuwa na elimu nyingi.
Wakati wa utoto wake, Julius Nyerere alichunga mifugo na alikuwa na maisha ya kawaida. Nyerere alikuwa mfuasi wa dini ya katoliki na watu waliomwona walisema alienda misa ya katoliki kila siku na hata wakati alikuwa mvulana, alifunga mara kwa mara. Kweli, mpaka alipokuwa na miaka kumi na mbili, Nyerere hakuwa na uzoefu na wazungu. Halafu aliingia shule huko mji wa Musoma, maili ishirini na sita kutoka nyumbani kwao (hili litaelezwa zaidi katika sehemu ya elimu yake.) Nyerere alibatizwa kuwa mkatoliki wakati alikuwa na miaka ishiniri. Nyerere alikua na kufika urefu wa futi tano na inchi sita na watu wote walisema alipenda sana kucheza na kufanya mizaha. Pia, wakati aliishi na kabila lake, alikata meno yake ya mbele na msumeno kuonyesha utamaduni wa kabila lake.
Maswali ya Ufahamu:

Habari na Abdallah Shelufumo, mmiliki wa Zefumo blogspot katika maadhimisho ya kumbukumbu za Baba wa Taifa, The World Hero Of Social Justice.



1. Nyerere alizaliwa nchi gani?
2. Nyerere aliishi miaka mingapi?
3. Nyerere alikuwa wa dini gani?

Sehemu ya Pili: Elimu
Julius Nyerere alienda Shule ya Msingi ya Serikali katika mji wa Musoma wakati alikuwa na miaka kumi na mbili. Alimaliza masomo ya miaka minne katika miaka mitatu kwa sababu alikuwa na akili sana, halafu alienda kusoma na Wavulana wa Shule ya Upili ya Serikali ya Tabora. Huko, alipata udhamini kwenda Chuo Kikuu cha Makerere. Ni muhimu kujua wakati alipata udhamini huo, Makerere kilikuwa chuo kikuu cha pekee katika Afrika ya Mashariki. Wakati alimaliza kusoma, alipata shahada.
Baada ya chuo kikuu, Nyerere alirudi Tanganyika na alifanya kazi katika Shule ya Upili ya St. Mary katika mji wa Tabora, katikati ya Tanganyika. Shule ya St. Mary ilikuwa shule ya kikatoliki. Huko, alifundisha masomo ya biolojia na
Kiingereza. Halafu, katika mwaka elfu moja, mia tisa na arobaini na tisa, alipata udhamini mwingine wa masomo. Wakati huu, aliweza kwenda chuo kikuu cha Edinburgh. Nilisoma vitu hivi katika wikipedia.com, na pia huko nilijifunza kwamba Nyerere alikuwa Mtanzania wa kwanza kusoma chuo kikuu cha nchi ya Wingereza na Mtanzania wa pili kupata digrii nje ya Afrika. Katika chuo kikuu cha Edinburgh, Nyerere alipata Shahada ya juu ya Sanaa katika Historia na Uchumi, mwaka elfu moja mia tisa, na hamsini na mbili. Katika Edinburgh, alisoma mkondo wa kufikiri unaoitwa “Fabian.” Mkondo wa “Fabian” wa kufikiri, ulijumuisha kundi la wataalamu wa Ujamaa wa Uingereza. Azimio la “Fabian” ni kuendeleza mawazo ya kijamaa kuongoa badala ya mapinduzi. Kwa hivyo, kwa sababu alijifundisha mawazo ya “Fabian,” alianza kufikiri mabadiliko mazuri sana yangepatikana ikiwa angeweza kuunganisha ujamaa na maisha ya Afrika. Wakati wa maisha yake, Nyerere aliitwa “mwalimu” kwa sababu ya kazi yake nyingi na elimu.
Maswali ya Ufahamu:
1. Kwa nini Nyerere alimaliza shule ya msingi mapema?
2. Nyerere alipata udhamini kwa nini?
3. Ni aina gani ya kufikiri aliyojifunza Nyerere huko chuo kikuu cha Edinburgh?

Sehemu ya Tatu: Ndoa na Familia
Wakati Julius Nyerere alikuwa mwalimu, na kabla ya maisha yake ya mwanasiasa, alioa mwanamke aliyeitwa Maria Magige. Maria alitoka kabila tofauti. Wanahistoria walisema alioa mwanamke wa kabila lingine kuonyesha dunia ilikuwa muhimu sana kusahau tofauti baina ya makabila na kusaidia umoja. Maria alimiliki duka dogo katika mtaa wa wenyeji wa Dar es Salaam. Pia, alikuwa rais wa Halmashauri ya Wanawake ya Tanganyika. Pamoja na Nyerere, alizaa watoto wanane, na leo watano wanaishi huko mjini Dar es Salaam.
Maswali ya Ufahamu:
1. Mke wa Nyerere alifanya kazi gani kabla ya kukutana na Nyerere?
2. Nyerere alikuwa na watoto wangapi?
3. Nyerere alifanya nini kujaribu kupata umoja baina ya makabila?

Sehemu ya Nne: Mchango Katika Jamii
Mchango mkuu wa Nyerere katika jamii ni kazi aliyofanyia serikali. Lakini kwanza nitaeleza kazi yake ya kufundisha. Nyerere alikuwa mwalimu wa historia, Kiingereza, na Kiswahili katika chuo cha St. Francis karibu na mji wa Dar es Salaam katika nchi ya Tanganyika. Huko, alianza shughuli ya siasa wakati alianza mradi wa TANU (Tanganyika African National Union) kupigania uhuru kwa nchi ya Tanganyika. Katika mwaka mmoja tu, TANU ilikuwa na watu wengi wapya na ilikuwa kiongozi wa miradi ya siasa katika Tanganyika. Kwa sababu Nyerere alianza kujihusisha na siasa, kwa ghafla alihitaji kuamua baina ya maisha ya mwalimu au maisha ya mwanasiasa. Watu wanasema Nyerere alisema “nilichagua kuwa mwalimu na ni ajali kwamba mimi ni mwanasiasa.” Alijiuzulu kutoka kufundisha, na Julius Nyerere alikuwa mwanasiasa kwa maisha yake.
Alisafiri ndani ya Tanganyika kusema na watu wengi na viongozi tofauti, kujaribu kupata msaada kwa harakati za uhuru wa Tanganyika. Katika mwaka elfu moja, mia tisa na hamsini na nne, alifaulu kuunganisha jamii mbalimbali kitaifa pamoja kusaidia harakati za uhuru. Nyerere alikuwa na ufarisi wa kusema uliomsaidia wakati alisema na UN (Umoja wa Mataifa) kuhusu uhuru wa Tanganyika. Katika mwaka elfu moja, mia tisa na hamsini na nane, aljiunga na Colonial Legislative na alishinda uchaguzi wa Waziri Mkuu katika mwaka elfu moja, mia tisa na sitini.
Nyerere alikuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Tanganyika mwezi wa kumi na mbili, tarehe tisa, mwaka elfu moja, mia tisa na sitini na moja, mwaka wa kwanza wa kujitawala kwa Tanganyika. Mwaka mmoja ulipita na Nyerere alishinda uchaguzi kuwa rais wa Tanganyika katika mwaka elfu moja, mia tisa, sitini na mbili, mwaka wa uhuru wa Tanganyika, jamhuri mpya. Pia, ni muhimu kujua kwamba Nyerere alifaulu kuunganisha kisiwa cha Zanzibar na Tanganyika bara pamoja kuunda nchi ya Tanzania katika mwaka elfu moja, mia tisa, sitini na nne, baada ya mapigano huko Zanzibar yaliyomaliza utawala wa Jamshid bin Abdullah, kiongozi wa Zanzibar.
Julius Nyerere aliendelea kuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania mpaka mwaka elfu moja, mia tisa, na themanini na tano. Wakati alikuwa rais, Nyerere alikuwa na matatizo mengi kwa sababu mwaka elfu moja, mia tisa na sitini, Tanzania ilikuwa nchi maskini sana kulinganisha na nchi zingine za dunia. Tanzania ilikuwa na deni kubwa sana na vitu viliongezeka bei. Kusaidia nchi yake, Nyerere aliamua kujaribu ujamaa na maisha ya pamoja vijijini, na utaifishaji. Aliandika dhana zake katika Azimio la Arusha la Mwaka elfu moja, mia tisa, sitini na saba, lililosema kuhusu maendeleo ya mashamba. Watu walihimizwa kuishi na kufanya kazi pamoja katika vijiji vilivyokusudiwa kusambaza desturi ya utamaduni wa Tanzania na kuunda umoja. Watu wanafikiri Nyerere alishinda matatizo mengi ya Tanzania na aliunda jamii ya umoja huko.
Baada ya shughuli ya Rais, Nyerere aliendelea kusaidia jamii yake. Alikuwa mwenyekiti wa Kundi: Chama cha Mapinduzi (CCM). Baada ya miaka michache, aliacha shughuli yake ya mwanasiasa kwa sababu alikuwa mzee. Alipumzika katika shamba lake huko Butiama, mjini alipozaliwa. Katika mwaka elfu moja, mia tisa na tisini, aliacha kuwa mwenyekiti wa CCM lakini aliendelea kufanya kazi ya haki za kibinadamu. Kwa mfano, katika mwaka elfu moja, mia tisa na tisini na sita, alikuwa mwamuzi mkuu wakati wa ugomvi katika nchi ya Burundi. Kwa bahati mbaya, alipata ugonjwa wa kansa ya leukemia, na alikufa mjini London mwezi wa kumi, tarehe kumi na nne, mwaka elfu moja, mia tisa, tisini na tisa.
Maswali ya Ufahamu:
1. Nyerere alikuwa rais wa Tanzania kati ya miaka gani?
2. Ni kisiwa kipi Nyerere aliunganisha na Tanganyika kuwa Tanzania?
3. Baada ya kazi ya rais, Nyerere alifanya nini?

Sehemu ya Tano: Maoni Yangu Kumhusu
Kwanza, ningesema Julius Nyerere alikuwa mtu wa athari kubwa sana. Kupitia wajibu wake wa kutetea haki za kibinadamu katika nchi yake ya Tanzania na katika dunia yote, alielimisha watu wengi. Julius Nyerere alifanya kazi tofauti: alikuwa mwalimu na mwanasiasa, lakini katika kazi zote, alijaribu kufanya jamii bora. Nyerere alikuwa mwanasiasa wa kanuni na akili sana. Alitumia ubongo wake kusaidia watu wa Tanzania kuishi maisha bora. Pia, alikuwa mwaminifu, kwa sababu wakati alikuwa rais alitumia msaada wote kusaidia Tanzania. Nyerere alikuwa na elimu nyingi, na kwa hivyo aliweza kusema waziwazi na kuandika katiba muhimu. Utafiti wangu uliniambia kuwa Nyerere alikuwa tayari kila siku kufanya kazi na vyama tofauti sana, na alisikia maoni ya watu wote. Tunaweza kuona alifanya kazi na Uingereza kusaidia watu wake. Pia, alikuwa sababu kubwa sana ya Tanzania kupata uhuru.
Maswali ya Ufahamu:
1. Kazi mbili tofauti za Nyerere zilikuwa nini?
2. Nilisema nini kuhusu kazi tofauti ya Nyerere?
3. Kwa sababu Nyerere alipata elimu nyingi, aliweza kufanya nini?

Sehemu ya Mwisho: Maswali ya Mjadala
1. Unafikiri kuwa mmoja wa watoto ishirini na sita kuliathirije Nyerere?
2. Kwa maoni yako, nini ni mchango mkubwa wa Nyerere katika jamii?
3. Unakubalina na dhana za Nyerere kuhusu Ujamaa?
4. Unafikiri nini katika maisha ya Nyerere kilimfanya kutaka kusaidia dunia?
5. Kwa nini Nyerere aliweza kuipata Zanzibar?
6. Unafikiri dini ya Katoliki ilimsaidia Nyerere?
7. Kwa maoni yako, elimu ni muhimu kwa nini?
8. Kwa nini Nyerere hakuona wazungu mpaka alipokuwa na miaka kumi na mbili?
9. Kwa nini Nyerere alikufa? Leo, kuna tiba kwa ugonjwa wake?
10. Je, unakubalina na maoni yangu kumhusu?

Marejeleo

“Julius Nyerere.” Wikipedia: The Free Encyclopedia. 10 May 2007. Wikimedia Foundation, Inc. 12 May 2007. .
Robbins, James. “Julius Nyerere: The conscience of Africa.” 14 October 1999. BBC World: Africa. 12 May 2007. .
Smith, Mark. “Julius Nyerere, Lifelong Learning and Informal Education.” 20 May 2007. Infed. 23 May 2007. .
Simmons, Charles E. “President Julius Nyerere: A Great Teacher and Devoted African Leader.” 12 May 2007. .

No related posts.